Mbunge wa Jimbo la Rufiji Mkoani Pwani tarehe 8 April 2017, amefanya ziara ya kujionea ubovu wa Barabara ya kuelekea Halmashauri ya wilaya, Makao Makuu ya Wilaya Utete baada
tuu ya kuingia Nchini.
Amesema Barabara hiyo ni mbovu na haifai, "tuwakumbushe
wananchi kuwa, nimeikumbusha serikali mara nyingi sana kuhusu ubovu wa
Barabara hii katika kila kikao cha Bunge kuliko Mbunge yeyote, Mbunge
wa CCM wa aina yangu ya Uchapa kazi, iwapo
nitashindwa kulisimamia Jambo, ni Ngumu sana kwa Mtu mwengine kuliweza,
kwa maana, jukumu nililokabidhiwa na wananchi ninalitendea Haki
ipasavyo kwa mapenzi ya Chama changu, mapenzi ya Warufiji wote bila
kujali itikadi zao"
Amesema Tarehe 3March.mwaka huu alitumia nafasi ya kuzungumza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania "juu ya vitu
nilivyomuomba ni Barabara ya Nyamwage -Utete, pamoja na Ikwiriri-Mwaseni
96km, alituahidi Ikwiriri tarehe 3, kuwa ataanza na Nyamwage Utete,
33km kabla ya 2020 iwe imekamilika. Tuendelee kumuombea Afya Njema Rais
wetu aweze kutekeleza ahadi hii" mheshimiwa mbunge ameongeza kuwa maumivu haya ni ya wanarufiji wote,
huduma za Afya kuelekea Hospitali yetu ya wilaya ni sawa na hakuna
kwasasa; sababu karibu ya 70% ya wananchi wote wa RUFIJI,wanaishi Nje ya
Makao makuu ya wilaya Utete,
Hali ni Mbaya; Ambulance haiwezi tembea
mwendo wa kasi kuwaisha mgonjwa, hata ikitokea dharura huwezi kuiwahi.
Mwendo wa Km 33 huweza kuchukua mpaka 2-4hrs barabara ikiharibika zaidi.
Ninaimani na Rais wangu Magufuli, Ninaimani kilio cha Warufiji kimepata suluhisho.. mheshimiwa Mohamedi Mchengerwa ameyasema hayo pamoja na mambo mengine ya kuhimiza maendereo na kutembelea miradi mbalimbali kubwa ni kujionea usumbufu wanao upata watumiaji wa barabara ya Nyamwage - Utete.
Kwa Taarifa mbalimbali za Kitaifa Kimataifa Michezo na Burudani tembelea shemsangablogs
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
-
Katibu Tawala Msaidizi wa Mkoa wa Pwani Shangwe Twamala akikagua baadhi ya bidhazaa za wajasiliamali wanawake waliohudhuria katika mkut...
-
Baba yake mzazi amefariki dunia usiku wa kuamkia leo. Meneja wake, Jahz Zamba, ameiambia Bongo5 kuwa Mzee Damian amefariki dunia baada ...
-
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Dkt. Harrison G. Mwakyembe (Mb), Jana tarehe 03 Mei, 2017 amekuwa mgeni rasmi kweny...

No comments:
Post a Comment